Mambo ya Kufanya na Mambo ya Kuepuka Baada ya Kutoa Mimba

Mambo ya Kufanya na Mambo ya Kuepuka Baada ya Kutoa Mimba

Utoaji mimba huwa inafanyika kwa njia ya kutumia vidonge (1) au kwa njia ya kufyonza (kunyonya) (2) – ni utaratibu ambao unahitaji muda na uangalifu wakutosha ili kupona vizuri. Ingawa utoaji mimba kwa njia ya dawa na ile ya kufyonza kwa ujumla ni salama unapofanywa na/chini ya uangalizi wa daktari mwenye vigezo, na ingawa mchakato wa kupona si mgumu ikilinganishwa na taratibu zingine, bado ni muhimu kupata usaidizi wa karibu baada ya kutoa mimba ili kuepuka matatizo yoyote. Zaidi ya hayo, ni muhimu kujua jinsi ya kujitunza ili kurahisisha mchakato wa kupona baada ya kutoa mimba, nje ya huduma zinazotolewa na daktari. Kwa watu wengi, matatizo ya baada ya kutoa mimba ni nadra na madhara madogo tu hupatikana. Lakini, linapokuja suala la kudhibiti athari hizi ndogo, ukosefu wa taarifa juu ya nini cha kufanya nini usifanye unaweza kuongeza uwezekano wa kupata matatizo. Taarifa ifuatayo ni muhimu katika kubainisha mambo yakufanya na yale usiyopaswa kufanya baada ya kutoa mimba ili kuhakikisha kwamba unapona vizuri.

Mambo ya Kufanya Baada ya Kutoa Mimba

Ushauri juu ya upangaji uzazi ni miongoni mwa mambo muhimu unayoweza kupatiwa kama usaidizi kutoka kwa daktari wako au mshauri wa matibabu. Kwa mujibu wa Paula H Bednarek, MD, MPH, ushauri nasaha wa upangaji uzazi hujumuisha kupitia upya mapendekezo yako ya njia za uzazi wa mpango na kujifunza njia nyingine ili uweze kuchagua njia iliyo bora zaidi kwa muda mfupi na mrefu (3). Upevukaji kwa kawaida hufanyika kwa siku 21 hadi 29 baada ya kutoa mimba, kwa hiyo ushauri wa upangaji uzazi unaweza kusaidia sana baada ya kutoa mimba kwani hukuruhusu kupanga na kuzuia mimba inayoweza kutokea ukiwa bado katika mchakato wa kupona (3). Ni vyema kushauriana na daktari au mshauri wa matibabu kuhusu ushauri wa upangaji uzazi baada ya utoaji mimba ikiwa bado hujafanya hivyo.

Aidha, zipo baadhi ya hatua za kuchukua ili kujitunza ukiwa nyumbani mara baada ya kutoa mimba. Kwa mujibu wa Laini ya afya , maudhi au athari mbaya unazoweza kupata baada ya kutoa mimba ni kama vile maumivu ya tumbo, uchovu na kichefuchefu (4). Unaweza kufanya mazoezi ya kujitunza mwenyewe na kupunguza athari hizi kupitia njia kama vile kutumia pedi za joto kupunguza maumivu ya tumbo, kunywa maji haswa wakati una kichefuchefu, na kutumia siku kadhaa kukaa nyumbani na kupumzika ili kuondoa uchovu (4).

Linapokuja suala la dawa, ni vema kutumia dawa zilizo pendekezwa na daktari/mtoa huduma wa afya, jambo hili ni muhimu kuzingatiwa mara baada ya kutoa mimba. Shirika la Planned Parenthood pia linapendekeza dawa kadhaa muhimu, kama vile ibuprofen na Norco kwaajili ya kutibu maumivu na kuhara (5). Hata hivyo, linapokuja suala la dawa, ni vema daima kuwasiliana na daktari wako au mfamasia kuhusu dawa yoyote unayotaka kutumia ili kupunguza athari.

Pia inashauriwa ufuatilie dalili zako na umjulishe daktari wako mara moja ikiwa utaona dalili isiyo ya kawaida. Maumivu makali/Maumivu makali ya tumbo, kutokwa na damu na homa kali inaweza kuwa dalili ya matatizo, ni muhimu kumjulisha daktari wako dalili kama hizi ili kupata matibabu mapema zaidi. Unaweza kutambua kuwa damu inayotoka ni nyingi kupita kiasi ikiwa utatumia pedi mbili kubwa kila baada ya saa kwa saa mbili mfululizo, na homa ya nyuzi 100.4 Fahrenheit (au nyuzi 38 Celsius) pia inachukuliwa kuwa athari mbaya zaidi (5). Inaweza kuwa ngumu kufahamu endapo maumivu uliyonayo ni makubwa kupita kiasi, lakini ikiwa unaona kwamba unakabiliwa na kile unachokiona kuwa maumivu makali ya tumbu, unapaswa kuwasiliana na daktari wako.

Pia ni muhimu kutambua kwamba mchakato wa utoaji mimba unaweza kupelekea msongo wa kihisia. Njia nyingine ya kujitunza unayoweza kutumia katika mchakato wako wa kupata nafuu ni kuwasiliana na watu wako wa karibu ambao wanaweza kukusaidia kihisia. Ni muhimu kuepuka kitu chochote cha kusumbua kama vile kazi au wasiwasi wowote katika wiki ya kwanza baada ya kutoa mimba ili kukuwezesha kupona kimwili na kihisia.

Mambo ya Kuepuka Baada ya Kutoa Mimba

Kurudi kazini, kufanya mazoezi mazito au kujihusisha na shughuli nyingine ngumu katika wiki ya kwanza baada ya utoaji wa mimba ni jambo lisilo faa. Hii ni kwa sababu shughuli nyingi za mwili mara baada ya utoaji wa mimba zinaweza kusababisha kutokwa na damu nyingi na maumivu makali ya tumbo hivyo kuchelewesha mchakato wa kupona (6). Jambo lingine linaloweza kuchelewesha mchakato wa kupona ni maambukizi. Inapendekezwa kuwa uepuke kukaa katika maeneo yenye maji maji kama vile bafuni au kwenye bwawa la kuogelea kwani jambo hili laweza kusababisha maambukizi (7). Epuka kufanya ngono au kuingiza kisodo kwenye uke, vikombe vya hedhi au kifaa kingine chochote kwenye uke wiki mbili baada ya utoaji mimba kwani hii inaweza kupelekea maambukizi (7). Ikiwa unatumia NuvaRing kama njia yako ya upangaji uzazi waweza kuendelea kwani njia hii haileti maambukizi.

Jambo jingine la kuepuka baada ya utoaji mimba ni matumizi ya dawa za antibiotiki (isipokuwa kwa ushauri wa daktari). Usitumie dawa hizi isipokuwa umepata maambukizi na daktari amekushauri utumie (8). Ikiwa daktari atakuandikia dawa za antibiotiki, hunabudi kutumia ingawa zitafanya uchelewe kupona.

Kwa ujumla, licha ya athari nyingine ndogo, mchakato wa kupona baada ya utoaji wa mimba haupaswi kuwa mgumu sana. Changamoto nyingi zinaweza kupata suluhu kwa kupata muda mzuri wa kupumzika, kupata uangalizi mzuri na kutumia dawa. Maadamu unawasiliana na daktari wako na unajitunza vyema kulingana na ushauri wake na kufuata dondoo zilizotolewa hapo juu, ni hakika utapona haraka.