Utokaji mimba usio kamili

Utokaji Mimba Usiokamilika: Dalili na Nini Unapaswa Kufanya

Utoaji mimba ni salama, ni miongoni mwa taratibu za kitabibu, na unaweza kuwa uchaguzi wa kuokoa maisha kwa watu ambao hawataki kubeba mimba. Hata hivyo, kama ilivyo kwa dawa zote, kuna hatari fulani.

Utokaji mimba usio kamili hutokea wakati utaratibu wa kutoa mimba umefanikiwa kwa kiasi kidogo. Ingawa mimba hutoka, baadhi ya tishu na mabaki ya kiumbe hubaki kwenye mwili.

Hatari ya utokaji mimba usio kamili baada ya kuachishwa kwa matibabu ni ndogo lakini huongeza baadaye mtu anapokuwa mjamzito. Hata hivyo kuna uwezekano mdogo wa kutokea kwa Utokaji mimba usio kamili endapo utafanyiwa upasuaji.

Ni muhimu kwa wale wanaofikiria kutoa mimba kujisikia salama pia nivema watafute taarifa zote zinazo hitajika kisha wafanye uchaguzi. Pia ni muhimu kwa walio toa mimba bila mafanikio kujua dalili, na kuchukua hatua.

Dalili za Utokaji Mimba Kutokamilika

Baada ya utaratibu wa kutoa mimba, ikiwa utapata moja ya dalili zifuatazo inaweza kuashiria kuwa utokaji mimba hauja kamilika:

  • Kutokwa na damu nyingi hali inayo pelekea kubadili taulo za kike kila saa, au kuganda kwa damu.
  • Kutokwa na damu mara kwa mara ambayo haipungui na hudumu zaidi ya wiki tatu.
  • Maumivu makali sana ya tumbo, au maumivu mengine ambayo huchukua muda mrefu.
  • Homa kali ambayo hudumu kwa zaidi ya siku mbili.

Ikiwa unapata mojawapo ya dalili hizo, usiogope, haimaanishi kuwa umetoa mimba isiyo kamili, huenda mwili unakabiliana na mabadiliko. Lakini, ikiwa utoaji mimba hauku kamilika, kuna njia mbalimbali za kufuata hivyo unashauriwa kufanya vipimo kisha utapatiwa matibabu ambayo ni rahisi na yanapatikana.

Nifanye Nini Ikiwa Ninafikiri Utoaji Mimba Wangu Haujakamilika?

Ikiwa unafikiri mimba yako haijatoka kikamilifu, ni muhimu kuwasiliana na daktari au kliniki ya ujauzito mara moja. Kadiri vipimo na matibabu yatakavyo fanyika mapema, ndivyo dalili zitakavyo toweka mapema. Pia matibabu yatazuia maambukizi au matatizo mengine makubwa zaidi.

Kutibu tatizo la utokaji mimba usio kamili ni halali kila mahali ikiwemo katika nchi ambazo ni kinyume cha sheria kutoa mimba kama sehemu matibabu. Si lazima uwaambie wataalamu wa afya kwamba ulipanga kutoa mimba kwa kuwa hakuna vipimo vya kubaini hili. Mahali popote kwenye vifaa vya kusaidia wale walio na uterasi na kuharibika kwa mimba kunaweza pia kusaidia wale wenye changamoto ya utokaji mimba usio kamili.

Vipimo vitafanyika baada ya kujadili dalili zako na daktari ambaye pia anaweza kuhitaji uchunguzi wa ultrasound, uchunguzi wa pelvic, uchunguzi wa rectal, au ukaguzi wa tumbo. Matibabu mara nyingi huwa ni vidongeviwili vya ziada vya Misoprostol, lakini pia vinaweza kujumuisha kuondoa tishu zilizobaki. Dalili zote zinapaswa kutoweka muda mfupi baada ya kupata matibabu.

Baada ya matibabu

Kutoa mimba kunaweza kuleta hisia kali, hasa ikiwa mtoaji alikumbana na changamoto kipindi cha utoaji. Kumbuka kuwa una haki ya kufanya maamuzi kuhusu mwili wako. Ukiweza, changamana na watu wanaokupenda na wanaoweza kukutunza. Kupumzika na kutunza afya yako ya akili ni muhimu kama vile kutunza afya yako ya kimwili.